MAMBO YA MUNGU


ushuda wa kweli. 

usikate tamaa


Niliingia kwenye Ukristo nilipofikisha miaka 18. Nilizaliwa kusini

mwa Urusi. Nilimpenda sana Yesu, na nikawa na bidii sana

Kanisani, nikabatizwa kwa Roho Mtakatifu na nikawa nawashuhudia

watu Injili. Mungu amenibariki sana.

Mungu aliponibatiza kwa Roho Mtakatifu nilipata shauku kubwa

sana ya kuwashuhudia watu habari za Yesu. Nilikuwa nikiongea

Habari Njema za Yesu karibu kila siku. Nilijihisi niko karibu sana na

Mungu. Nilitumia saa nyingi kuomba na kusoma Biblia.

Wakati fulani nilipatwa na jinamizi. Niliota kuwa ibilisi ananifukuza.

Aliapa kuwa ni lazima atanipata. Nilipozinduka usiku ule, hofu

haikuondoka. Badala yake ilizidi kuongezeka. Hofu iliongezeka sana

kiasi kwamba nikawa nimechanganyikiwa kabisa. Nilijua kuwa niko

katikati ya uovu. Nilikuwa chumbani kwangu, lakini ilionekana kana

kwamba niko mahali pengine kabisa. Nilianza kuhangaika kuomba

na kumsifu Mungu. Hili lilikuwa ni jambo pekee lililonifanya nibakie

na akili zangu timamu. Niliomba karibia usiku kucha. Ile hali ya

uovu ilikuja kuondoka asubuhi.

Nilipomsimulia jambo lile mmoja wa wamisionari wa Kimarekani

kanisani kwangu, aliniambia kuwa ibilisi amefungwa na kuwa

hana uwezo wa kumdhuru Mkristo yeyote. Nilikuwa sijawahi

kufundishwa chochote kuhusiana na vita vya kiroho na sikujua

kuwa nilitakiwa kufanya kitu ili kumpinga adui. Nimekuja kujifunza

ukweli huo kwa njia ngumu kabisa. Ni miaka mitatu baadaye ndipo

nilipofahamu kuwa ibilisi yu hai na yuko duniani; na anachukia sana

na kushindana na kila mmoja anayeamua kuyatoa maisha yake kwa

Yesu Kristo.

Muda mfupi baada ya kupata ubatizo wa Roho Mtakatifu, kwa ndani

moyoni, nilianza kujiona kuwa mimi nilikuwa mtu maalum sana

kwa Mungu kuliko Mkristo mwingine yeyote au watu wengine.

Nilianza kuhisi hivyo kwa sababu ya baraka zote za kimwili na

kiroho alizonipa Mungu. Kazi yangu ya ukufunzi ilikuwa inakua

kule Urusi; nilipokea fedha kwa ajili ya kusafiri ng’ambo, na zaidi

ya hapo, nilipewa skolashipu kamili ya kwenda kusoma Chuo Kikuu

cha Columbia kule New York.

Siku moja wakati nikiomba, Mungu aliniambia kuwa ninatakiwa

kutubu. Mungu alinionya kuhusiana na majivuno yangu na

kuniambia nitubu, vinginevyo NINGEANGUKA. Alisema kuwa mimi

sikuwa mtu maalum kuliko mtu mwingine yeyote. Pia aliniambia

niache kuwahukumu wengine. Kwa bahati mbaya, mimi nilikuwa

nimesisimka zaidi kutokana na ukweli kwamba Mungu anasema

nami badala ya ukweli kwamba nilitakiwa kumtii na kufanya kile

anachoniambia.

Kuishi katika jiji la New York...

Miaka minne iliyopita, toka tarehe ya kuandikwa kwa ushuhuda

huu, nilienda New York ili kusomea shahada ya pili kwenye Chuo

Kikuu cha Columbia. Nikiwa New York, mambo hayakwenda kama

nilivyokuwa nimetarajia. Nilikuwa na vita vikubwa na sikuelewa

kwa nini Mungu aliruhusu nipitie mateso kiasi hicho. Japokuwa

Mungu alinibariki sana kwa skolashipu kamili kwenda kusomea

Columbia, sikumwamini na wala sikumshukuru wakati wa mapito

yangu magumu. Badala yake, nilipachukia New York na Columbia

na nikaanza kunung’unika na kulalamika sana.

Huu ulikuwa ndio mwanzo wa kuanguka kwangu. Niliingiwa na

huzuni kubwa sana na nikawa katika maumivu na hofu kubwa.

Nilifunga, nikaomba mara kwa mara, nikasoma Biblia, nikaenda

kanisani, lakini maumivu na hofu ile havikuondoka! Hali ile

ilikuwa inatia uchungu moyo wangu kiasi kwamba ikawa ni vigumu

kwangu kutembea au kuzungumza. Kila dakika ilihitaji nguvu

sana. Ilikuwa ni kama vile mtu ananivuta chini na kunizuia kupiga

hatua. Muda wote nilikuwa nanyanyaswa na ibilisi ambaye alikuwa

akiniambia kuwa mimi nimeshashindwa kabisa.

Baada ya mwaka mzima wa mateso yangu, Mungu alinivuta tena

kwake kwa muda mfupi. Alizungumza nami na nikaandika maneno

yake kwenye kitabu changu cha kumbukumbu. Ni kwa miaka miwili

tu ndio nilielewa kile alichokuwa ameniambia. Mungu aliniambia

kuwa nitapitia majaribu makali sana na kwamba ningeteseka sana,

lakini aliahidi kunivusha katika yote hayo na kuleta mabadiliko

yenye matunda mema ndani yangu.

Wakati nilipokuwa naisikia sauti ya Mungu, nilikuwa naweza pia

kusikia sauti za mapepo. Nilikuwa sijui kabisa kwamba mapepo

yanaweza kuiga sauti ya Mungu ili kuwadanganya Wakristo.

Sikujua kuwa natakiwa kulijaribu kila neno kwa njia ya Biblia.

Ndiyo maana, niliposikia kuwa ningeenda kufanya mafunzo ya

vitendo kwenye Benki ya Dunia na kwamba ningekutana na

mume wangu wa baadaye kule D.C, niliamini kuwa hayo yanatoka

kwa Mungu. Kumbe pepo alikuwa anasema na tamaa zangu za

kimwili. Niliyapenda maneno hayo na nikayaamini. Nilikuwa na

mashaka, lakini pia nilidhani kwamba Mungu hawezi kuruhusu pepo

anidanganye.

Muda mfupi baada ya hapo, rafiki yangu pekee Mkristo wa New

York aliondoka kwenda kwenye mapumziko ya majira ya joto.

Nilibakia peke yangu. Japokuwa nilikuwa nimeshakaa kwenye

jiji hilo kwa mwaka mzima, bado sikuwa na marafiki wa Kikristo.

Nilihudhuria kanisani, lakini sikuwa namfahamu yeyote pale.

Nilijawa na huzuni zaidi. Nilikuwa peke yangu kabisa na sikuwa na

mtu wa kumshirikisha mashindano yangu. Nilidhani kuwa Mungu

alikuwa hajali na hakunipenda tena kwa kuwa hakujibu maombi

yangu ya kupata kanisa na kuwa na marafiki wa Kikristo. Niliishiwa

na nguvu kabisa pale niliposhindwa kwenye usaili kwenye Benki

ya Dunia na kukosa kazi. Sikuelewa kwa nini Mungu aliruhusu

pepo anidanganye. Sikuwa na hamu ya kuishi tena na nikaanza

kuwaza juu ya kujiua! Sikuweza kabisa kustahimili maumivu yangu

yasiyokoma.

Kisha nilitambua kuwa nisingeweza kufa kwa sababu nikijiua

ningeenda jehanamu na kutumbukia kwenye mateso makubwa

zaidi, tena ya milele! Nikajiona kama mtu aliyenaswa. Kuishi sitaki

lakini wakati huohuo kujiua nako siwezi. Nilijihisi kama vile niko

jehanamu. Maumivu yalikuwa makali sana kiasi kwamba nilianza

kujikata kwa kisu, maana maumivu ya kimwili yalionekana kwangu

kuwa ni mepesi kuliko mateso ya moyoni mwangu. Uovu ulikuwa

wakati wote umenizunguka, ukipenya ubongo wangu, ukinitesa

moyo wangu, wakati wote ukiwa tayari kusema nami na kuniburuta

chini! Kadiri nilivyozidi kuomba na kusoma Biblia, ndivyo nilivyozidi

kuteswa na hizo sauti, na ndivyo maumivu yalivyozidi. Sikujua cha

kufanya na sikuwa na jinsi ya kuzuia!

Ndipo nilifanya jambo ambalo si la kawaida. Sikuwa na uwezo wa

kustahimili maumivu zaidi ya hapo, hivyo nikawa nimeanguka

kabisa. Nilijawa na hasira sana dhidi ya Mungu kiasi kwamba

nikamwambia aondoke kwangu na aachane nami! Nilimwambia

kuwa simpendi na sikuwa tayari kuzungumza naye tena wala kuwa

naye. Kwa kuwa nilikuwa ni mtu wa kuzungumza naye kila wakati,

ilibidi nijilazimishe sana kuacha kumfikiria. Niliacha kuomba na

kusoma Biblia. Nikaamua kufuata njia zangu mwenyewe. Sikuwa

najua sawasawa madhara ya hatua yangu hiyo. Sikujua kuwa

nilimwacha Mungu na kumfuata ibilisi. Sikutambua kuwa mtu huwa

ama yuko anamtumikia Mungu au anamtumikia shetani – hakuna

namna ya kusema ‘mimi siko kwa Mungu wala kwa shetani.’ Ukiwa

kwa Mungu unakuwa hauko kwa shetani. Ukiwa nje ya Mungu, moja

kwa moja unakuwa uko kwa shetani. Hakuna sehemu ya kati!

Hivi sasa ninatambua kwamba Mungu alikuwa muda wote

ananiangalia licha ya maamuzi yangu yote mabaya.

Katikati ya majira ya joto, nilipata kanisa na kuwa na marafiki

kadhaa. Hatimaye sasa nilikuwa na mtu wa kuzungumza naye

na angalau kutoka naye. New York ni sehemu ngumu sana kwa

Wakristo. Pia, hivi sasa ninatambua kuwa kumbe hata marafiki

zangu pale kanisani nao walikuwa wanapitia magumu mengi vilevile

kama mimi! Hata hivyo, kuwa wewe na kuombeana na kumtazama

Yesu yalikuwa ni mambo ambayo tulikuwa hatufanyi. Kutafuta

mafanikio ya kazi lilikuwa ndilo jambo tulilolipa umuhimu zaidi.

Jumapili moja nilikutana na mwanamume mmoja kanisani. Mara

moja nilivutiwa naye. Ninapotafakari sasa ... natambua kuwa mara

nilipoondoa macho yangu kwa Yesu, nilifanyika mtu rahisi sana

kushambuliwa na shetani. Hilo lilimpa nguvu juu yangu na kudhibiti

hisia zangu na mawazo yangu. Na kwa kuwa sikuwa na upendo kwa

Mungu moyoni mwangu, nilihitaji kitu mbadala. Nikawa nimevutika

kabisa kwa huyu mwanamume.

Pale nilipokuja kutambua kuwa uhusiano wangu naye hauwezi

kufika mbali, nilianza kumwomba Mungu na kusoma Biblia.

Hata hivyo, bado nikawa sikumwomba Mungu awe Bwana wa

maisha yangu tena. Nilitaka tu anisaidie kwenye matatizo yangu

niliyojisababishia mwenyewe. Kwa kule kutoyatoa maisha yangu

yote kwa Mungu, sikuwa na uwezo kabisa wa kuvunja ule uhusiano.

Sikujua wakati ule kwa nini sikuweza kumkatalia yule bwana

kunitumia mimi, na kumwambia ‘hapana’. Nilikuwa nimenaswa

kwenye hisia zangu mwenyewe na sikuwa na uwezo wa kutoka

humo. Nilijua kwa moyo wangu wote kuwa nilikuwa namtenda

Mungu dhambi.

Nilibakia nikiwa nimenaswa kwenye uhusiano huu kwa mwaka

mzima. Kwa kuwa huyu bwana hakuwa msomaji wa Biblia na

hakupenda kuzungumza kuhusu Mungu, mimi nami pia niliamua

kuacha kuyafanya hayo. Kwa hiyo, nikawa nimeenda mbali zaidi na

Mungu na hatimaye nikawa nimekuwa mwenyewe tu.

Baada ya mahafali yangu ya chuo, nilifanya kazi New York katika

kipindi cha majira ya joto. Nilipata kazi kwenye benki yenye

hadhi na nilikuwa na uwezo sana kwenye kazi yangu. Bosi wangu

aliniambia jinsi ambavyo alipenda kazi yangu na jinsi nilivyokuwa

bora na mwenye akili. Nilijawa na majivuno na kiburi hata zaidi.

Baada ya uhusiano wangu na yule bwana kuvunjika, nilijihisi kuwa

ninataka kugeukia kwenye kitu kingine ili kujaza uwazi uliotokea.

Bado nilikuwa najiona kuwa simhitaji Mungu. Nilikuwa bado nina

hasira naye kutokana na kutonipatia kile nilichohitaji. Ndipo kazi

yangu ikawa ndiyo mungu wangu. Nilimuabudu huyu mungu wangu

kwa bidii zote.

Kuishi Moscow…

Nilipoenda Moscow, nilipanga kufanya usaili na mabenki kumi

makubwa ya nje. Cha kushangaza, mambo yaligoma kabisa!

Sikuweza popote kupata kazi niliyoitaka! Najua sasa kuwa, sababu

mojawapo ya mimi kushindwa kwenye kila usaili ilikuwa ni tabia

yangu ya majivuno ambayo ilionekana kunisaidia sana wakati

nikiwa New York, lakini hakuna mtu aliyehitaji kiburi hiki kule

Moscow.

Niliishia kupata kazi ambayo niliichukia kabisa. Hata hivyo, ilibidi

niiache baada tu ya miezi mitatu. Niliweza kupata kazi nyingine

Moscow. Nilipoambiwa niache kazi yangu ya pili, kwa vile sikuwa

nafaa kabisa kwenye kazi hiyo, na pale nilipokataliwa kwenye

kila usaili niliofanya kule London, nilitambua kuwa Mungu alikuwa

anajaribu kila njia kunifanya nishtuke.

Nilipoteza kazi yangu Aprili (2004). Nilifanya usaili mara kadhaa,

lakini kazi sikupata. Kila jitihada ilikuwa haizai matunda kwangu!

Hatimaye Mungu alifanikiwa kuvuta umakini wangu. Nikaanza

kumwomba. Hata hivyo, nilijihisi kuwa hata nikitubu vipi, siwezi

kusamehewa. Nilipakua Biblia kutoka kwenye intaneti maana

nilishatupilia mbali Biblia zangu zote pale nilipoondoka New York.

Nikaanza kusoma Agano Jipya tena.

Siku moja, nilipojua kuwa usaili wangu wote umekwama, nilimlilia

Mungu ili anisaidie. Nilijiona sina tena matumaini kabisa.

Ndipo nilianza tena kusikia sauti ya ibilisi ikiniambia kuwa Mungu

hanipendi na hatanisamehe; na kwamba inabidi nijitupe kupitia

dirishani. Sauti ile ilikuwa ina ushawishi mkubwa na nguvu sana

kiasi kwamba nilidhani kuwa nitakuwa kichaa. Huku nikilia,

nilifungua Biblia na kuanza kusoma kwa sauti japokuwa nilikuwa

sielewi hata neno moja. Lakini sauti ile ikawa imetoweka!

Nilitambua kuwa nilikuwa nimemtenda dhambi Mungu sana na

nilihitaji kujua iwapo angenisamehe. Nikakumbuka hadithi za

kwenye Agano la Kale kuhusu Israeli – wafalme waliomtenda

dhambi Mungu, lakini wakatubu. Nikaanza kusoma hadithi zile.

Nikatambua kuwa majivuno yangu na kutotii zilikuwa ndizo dhambi

zangu kubwa mbili.

Katika kipindi cha kurudi kwangu kwa Mungu nilikutana na tovuti

yenye Shuhuda za Thamani. (www.precious-testimonies.com).

Nilisoma shuhuda karibu zote humo! Niliguswa sana na upendo

wa Mungu kwenye maisha ya watu mbalimbali. Niliguswa sana

na mateso na maumivu ambayo kila mmoja aliyapitia hadi kuja

kumpata Yesu Kristo. Lengo langu, nilikuwa nataka sana kujua

kama Mungu angeweza kunisamehe dhambi zangu.

Kupitia kwenye Biblia, na shuhuda zile, nilitambua kuwa sikuwa

nimempa Yesu maisha yangu yote na kwamba nilikuwa bado

nimeshikilia mambo yale niliyoyapenda na nilikuwa naogopa

kuyaachia na kumpatia Yesu. Pia nilitambua jinsi ambavyo

dhambi zangu zilimpatia shetani nguvu kubwa ya kuharibu maisha

yangu. Nilijifunza jinsi ilivyo kutembea kwenye njia ya ibilisi.

Sitakiubinafsi tena! Nilitaka kumtumikia Yesu japokuwa isingekuwa

rahisi na wakati mwingine ingekuwa vigumu sana. Lakini Yesu

hutoa uzima wa kweli na anajua kile kinachofaa kwa ajili yetu.

Mungu alikuwa na rehema na neema sana kwangu na Roho

Mtakatifu wake aliniongoza kwenye toba. Alihukumu majivuno

yangu na kukosa kwangu utii na uzinzi wangu. Tarehe 12 Juni,

2004, nilimpokea Yesu kama Bwana na Mwokozi wa maisha

yanguyote – si kwa sehemu yake tu! Nilimwambia achukue ndoto

na mapenzi yangu yote ya ubinafsi na aweke ndani yangu ndoto

na mapenzi yake. Nilimkabidhi hofu zangu zote. Nilimwambia

kuwa sikutaka tena kumtumikia shetani bali nataka kumtumikia

Yeye – Yesu. Maamuzi yangu yote ya nyuma yalinipeleka kwenye

kushindwa kabisa. Nilitaka sasa Yesu atawale maisha yangu na

kuyabadili apendavyo, na si vile ninavyotaka mimi.

Baada ya kufanya hivyo, nilijisikia faraja kubwa sana! Kwa mara ya

kwanza katika miaka mitatu, nilikuwa natembea barabarani huku

nikitabasamu na kupumua kwa uhuru tena. Nilijisikia mwepesi na

huru kabisa.

Nilikuwa nimeishi Moscow kwa karibu mwaka mzima, lakini nilikuwa

sina rafiki Mkristo hata mmoja. Kabla ya toba yangu, nilihudhuria

kanisa jingine lakini bado nilikuwa simfahamu hata mtu mmoja.

Kutokana na tabia yangu ya New York ya kutojiweka wazi, nilikuta

ni vigumu sana kuweka wazi mambo yangu ya moyoni kwa watu

wengine. Hii ndiyo sababu hakuna aliyejua kile nilichokuwa napitia;

na pia ndiyo sababu sikuwa na mtu wa kumweleza kuhusu mapito

yangu.

Baada ya uamuzi wangu huo, nilidhani kuwa ningeweza kurudi

kwa Mungu kwa nguvu za maombi yangu, toba na kusoma

Biblia mwenyewe. Lakini siku chache baada ya kuamua kumrudia

Mungu, nilihisi kama kuzimu yote imesimama kinyume nami!

Nilianza kuona kiumbe mwenye manywele mengi. Taswira hii

ilikuwa mbele za macho yangu muda wote kwa wiki kadhaa.

Nilikuwa ninaomba na kuomba na kusoma Biblia. Nilifunga

pia. Nilikiri damu ya Yesu juu yangu. Taswira hii mbaya wala

haikuondoka! Nilihisi kuwa ninachanganyikiwa. Usiku haikuwa rahisi

kulala. Sauti ilianza kuniambia tena kuwa Mungu hatanisamehe kwa

kuwa nimemkufuru Roho Mtakatifu na kutenda dhambi ambayo

Yesu hawezi kusamehe.

Siku moja niliamka nikiwa na uchungu na hasira. Nilihisi ule

mzigo na uzito tena. Nikaanza kumwomba Mungu anisamehe

na kumshukuru Yesu kwa kunifia. Lakini mashindano yangu

yakaendelea kuwa magumu zaidi na zaidi. Siku ile nilitambua kuwa

siwezi kushindana na ibilisi peke yangu. Nilihitaji msaada. Nilihitaji

sana mtu wa kuniombea.

Kweli imeshafunuliwa …

Pale nilipotambua kuwa nahitaji mtu wa kuniombea, niliamua

kupeleka mahitaji yangu ya maombi kwa watumishi wa tovuti

yaPrecious Testimonies. Watumishi hao si tu kwamba waliniombea,

bali pia walinipatia mwongozo muhimu sana kwa njia ya baruapepe.

Ilikuwa ni wao ndio walionifungua macho kuhusiana na ukweli

kwamba ibilisi yu hai na yuko duniani huku akifanya vita dhidi ya

Wakristo. Nilitambua kuwa yalikuwa ni mapepo ndiyo yaliyokuwa

yananiletea maumivu na mateso makubwa namna hiyo. Nimejifunza

pia kuwa ibilisi anawapepeta Wakristo wote kama ngano. Adui

aliwashambulia na kuwatesa Petro na Paulo na mitume wengine.

Anafanya hivyo hata leo kwa nguvu na ukali uleule!

Ulimwengu wa roho…

Nilipokuwa ninakandamizwa na adui mara baada ya kutubu

kwangu, Mungu alinifungua macho ili niweze kuona ulimwengu wa

roho. Kama nilivyosema, nilidhani kuwa ninachanganyikiwa pale

nilipoona kiumbe mwenye manywele mengi. Baada ya kutuma

mahitaji yangu ya maombi, nilijisikia amani kubwa. Nilijua kuwa

kuna mtu ameanza kuniombea.

Hata hivyo, niliendelea kuyaona mapepo yakinizunguka. Nilipoamka

siku iliyofuata, si tu kwamba niliweza kuyaona mapepo, bali pia

nilimwona malaika wangu. Taswira zilikuwa kama kioo. Nilikuwa

sina hofu hata kidogo. Niliweza kuona kwenye ulimwengu wa roho

kwa wiki kadhaa. Mungu alinifundisha masomo muhimu sana katika

kipindi hicho.

Somo la 1: Mapepo hayawezi kustahimili kusikia Neno la

Mungu.

Wakati fulani nilirudi nyumbani kutokea kanisani na nikawa nasoma

Maandiko. Niliinua macho na kuyaona mapepo kadhaa. Nikaanza

kumwomba Mungu anisaidie. Sikuwa nina hofu lakini nilikuwa tu

sijisikii amani kuyaona. Wakati nikiwa namwomba Mungu anisaidie,

nilisikia sauti moyoni mwangu ikisema, “Soma Maandiko.”

Nikauliza: “Nini?” Sauti ile ikarudia tena: “Soma Maandiko.” Nilitii

na nikaanza kusoma Maandiko. Lakini baada ya muda kidogo,

Mungu akaniambia: “Soma kwa sauti.” Nikawa kama

nimechanganyikiwa kidogo, lakini Mungu akarudia tena: “Soma

Maandiko kwa sauti.” Nilipoanza kusoma Maandiko kwa sauti

niliona kuwa mapepo yale yanafunika masikio yao kwa mikono yao

yenye makucha na kuanza kuhangaika kwa mateso makubwa. Hivi

ndivyo nilivyojifunza kuwa mapepo hayawezi kustahimili kusikia

Neno la Mungu. Neno la Mungu likitumika kwa imani na kweli, ni

silaha kubwa dhidi ya nguvu za giza.

Tangu hapo, nimejenga tabia ya kusoma Neno la Mungu kwa sauti.

Pia nimepakua kutoka kwenye intaneti Agano Jipya la sauti (lililo

katika fomati ya MP3). Nikiwa nyumbani, karibu muda wote huwa

nimefungulia Biblia hiyo. Huwa naisikiliza nikiwa nakula, napika,

najipamba, nk. Mara kadhaa Mungu amekuwa akielekeza umakini

wangu kwenye mistari ya muhimu sana na kunieleza maana yake

wakati nikiwa nakula au najiandaa kwenda kazini. Mwenzangu

mmoja aliniuliza ni rekodi ya aina gani hii ambayo huwa naisikiliza

karibu saa 24 kila siku. Nilimweleza na kumshirikisha sababu zangu

za kufanya hivyo, lakini najua kuwa hakunielewa kikamilifu.

Vilevile nilipakua Agano Jipya kwa ajili ya kompyuta yangu ya

mfukoni. Kila ninapopata nafasi, huwa najaribu kusikiliza Maandiko

niwapo kazini. Mara nyingi ninapopatwa na mashambulizi ya adui

nikiwa kazini, huwa naamua kusikiliza Biblia hiyo kama njia yangu

mojawapo ya kunisaidi kushinda vita.

Pia nilijifuza kwamba mapepo huteswa sana hasa na Kitabu cha

Ufunuo, na hususani sura ya 17, 18, 19, pale ambapo Maandiko

yanazungumzia kuhusu hatima yao ya mwisho. Hayawezi kabisa

kusikiliza mistari kuhusu Babeli ulioanguka na mistari kuhusu ibilisi

na manabii wake wa uongo kutupwa kwenye ziwa la moto.

Kuna mara kadhaa ambapo niliyatishia mapepo kuyasomea Kitabu

cha Ufunuo kama hayakuacha kunisumbua au kuondoka. Ni wazi

kuwa sikuyatishia tu, bali nilisoma sehemu hizo. Mbinu hii hata

hivyo si kwamba ndiyo jibu la kila kitu. Haikuhakikishii ushindi

kwenye kila shambulizi, lakini ni mbinu nzuri ya msaada upande

wetu. Mungu mara zote hunisaidia kupata mstari ambao unaweza

kunyamazisha kabisa sauti ya adui. Nimeshajifunza kuwa si kila

mstari utanyamazisha manyanyaso ya adui bali ni ile mistari

ambayo inahusiana moja kwa moja na tatizo lililopo. Ni kama ilivyo

kuinua upanga hewani na kupiga kushoto wakati adui yuko kulia.

Hiyo haisaidii kumshinda adui. Ni pale tu unapoelekeza mapigo

yako kwenye lengo ndipo utashinda mapambano. Hali ni ileile hata

kwenye mistari ya Biblia na uongo na unyanyasaji wa adui. Ndiyo

maana NI LAZIMA kujifunza Maandiko kwa bidii na kuweka mistari

kwenye kumbukumbu kichwani.

Katika majaribu ya Yesu ya siku 40 kule jangwani – pale shetani

alipomjaribu – je, Yesu alifanya nini? Alimjibu shetani kwa kutumia

mistari sahihi kutoka kwenye Neno la Mungu. Alishindana na

shetani kwa kutumia upanga wa Roho Mtakatifu, ambao ni Neno la

Mungu. Shetani anamnukulia Yesu Neno lakini si kikamilifu; anataja

nusu ukweli. Ukweli nusu mara zote huwa ni uongo uliokusudiwa

kudanganya wanadamu na kupoteza makusudi ya Mungu kwa ajili

ya wanadamu. Yesu alimnukulia shetani Kweli yote kwa 100% ...

na shetani hakuwa na kitu chochote cha kushindana na mbinu

ya mapambano ya Yesu. Shetani alishindwa kwa 100% kwenye

vita hivyo. Mungu hakuruhusu jambo hili liandikwe kwenye Biblia

kwa bahati tu ili kujaza nafasi. Shindana na mashambulizi ya

mapepo kwa kutumia kwa usahihi Neno la Mungu.

Lijue Neno ... Liamini Neno ... Fahamu lini pa kulitumia kwa

usahihi (usinukuu tu Neno nje ya uhalisia wa hali yako; mapepo

watakucheka!); kisha tamka Neno la Mungu kwa sauti, imba

nyimbo zinazotokana na Maandiko; omba Neno wakati wa maombi

yako na kuyaambia mapepo yanayokuzunguka, (japo huenda

hutakaa uyaone) – sikiliza Neno la Mungu linapoongelewa dhidi ya

matatizo yanayokukabili, lakini kwa mwongozo wa Roho Mtakatifu.

Mambo yote yanaweza kushindwa lakini haiwezekani kwa Neno la

Mungu kushindwa maana Roho Mtakatifu ndiye anayelifanya litende

kazi. Mungu hawezi kusema uongo; hivyo Neno la Mungu nalo

haliwezi kuongopa. Wanadamu hapa duniani wanaweza wasilielewe

Neno la Mungu, hivyo wakalitumia kimakosa katika hali zao, lakini

hilo haliwezi kutokea kwa msaada wa Roho Mtakatifu. Hilo kila mara

hutokea kwa sababu ya nguvu za kipepo na mawazo ya kimwili ya

wanadamu ambao hawana ufunuo kamili wa Neno la Mungu, au

huenda wamelipindisha bila wao kujua, na kulifanya liseme kitu

ambacho Mungu hajasema. Kama Mungu alivyoandika: "Mbingu na

nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe.” (Tazama:

Mt. 24:35; Mk 13:31; Lk 21:33). Mtu anapopokea ufunuo kamili

kwamba Yesu Kristo ndiye Neno, haishangazi basi kwamba

halitapita kamwe.

Somo la 2: Mapepo hujaribu muda wote kuingiza mawazo

maovu/ya udanganyifu kwenye akili yako.

Mara nyingi mapepo wanaficha sana udanganyifu wao kiasi kwamba

ni vigumu kutofautisha kati ya sauti na mawazo yao na yako. Hivyo,

kulisha ufahamu wako kwa Neno la Mungu kila wakati, kuomba na

kuwa mwangalifu ni mambo ya muhimu ili kuweza kutofautisha kati

ya mawazo yako na uongo wa adui.

Nilipojua ukweli juu ya hasira kali ya ibilisi na mapepo, nilianza

kutambua mengi ya mashambulizi yao yaliyofichika, hususani

mashambulizi ya kutaka kunishawishi nikubali uongo wao.

Nimegundua kuwa mambo mengi yanayokuja kwenye ufahamu

wangu hayatoki kwangu au kwa Roho Mtakatifu, bali ni kutoka kwa

mapepo.

Ukweli kwamba niliweza kuona jinsi ambavyo mapepo yanafanya

kazi kunizunguka mimi, kumenisaidia sana kutambua mashambulizi

yao na kupambana nao. Ni muhimu kabisa kutambua mashambulizi

yao mara tu yanapoanza na kutoyaruhusu kukamata akili yako.

Jambo la kwanza yanachofanya ni kupenyeza uongo kwenye akili

zetu. Kama uongo wowote ukikubaliwa na akili zetu, ni vigumu sana

kuja kuutambua baadaye na kupambana na mapepo. Si ajabu basi

Maandiko yanatuonya mara , yakitutaka kuwa macho kila wakati,

kuzifunga nia zetu, kukesha, kutofuatisha namna ya dunia hii bali

kufanywa upya nia zetu (kufanywa upya kwa Neno la Mungu).

Nimejifunza kuwa kudhibiti akili zangu ni jambo la lazima. Maana

silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata

kuangusha ngome; tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka,

kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira

ipate kumtii Kristo [Neno lake] (Tazama 2 Kor. 10:4-5). Ni

mashindano yasiyokoma kwangu kufanya kila wazo limtii Kristo

na kuharibu kila kitu ambacho mapepo yanajaribu kukiinua akilini

mwangu kinyume na elimu ya Kristo.

Ninakumbuka shambulizi moja ambapo akili yangu ilishambuliwa

kwa nguvu sana na adui na ilinibidi nisome Maandiko kwa sauti

mfululizo kwa saa kadhaa.

Mapepo yanaposhambulia akili, nimekuta pia kuwa kuna nguvu

sana ninapoyajulisha kuwa nimeshajua kwamba yananishambulia.

Kwa kuwa menyewe hupenda kutenda kazi zao kwa kificho

na hayapendi kuwekwa wazi, njia mojawapo yenye nguvu ya

kupambana nayo ni kuyafanya yajue kuwa umeyatambua.

Nakumbuka pia mapambano fulani ambapo nilijihisi kuwa

siwezi kabisa kuzuia manyanyaso ya adui. Mapepo yaliendelea

kunikumbusha jinsi ambavyo niliudhiwa na kuaibishwa kazini.

Yalikuwa yakiingiza akilini mwangu kila aina ya uongo yakitaka

kunifanya niwachukie wafanyakazi wenzangu na kumwasi

Mungu. Nilijaribu kila njia iliyokuwa ikiwashinda hapo kabla

kwenye mashambulizi mengine, lakini haikuwezekana. Yalikuwa

ni mashambulizi mfululizo ambayo sikuweza kupata namna ya

kushinda. Kisha asubuhi moja, mapepo yalipofanya mashambulizi

yao kama kawaida, Mungu alinifundisha mbinu yenye nguvu.

Niliyaambia mapepo kwamba, kila mara yatakaponikumbusha

jambo linalohusu kunyanyaswa kwangu na wafanyakazi wenzangu,

basi mimi nitawaombea, nitayafunga mapepo yanayowadhibiti

na nitamwomba Mungu awaimarishe malaika wa vita ambao

wanapigana kinyume na mapepo yale. Kweli kabisa baada ya

kuhakikisha kuwa nilikuwa sitanii juu ya kuwaombea wafanyakazi

wenzangu, mara moja mapepo yaliondoka na nikawa nimeshinda

vita ile. Ni wazi kuwa hata sasa bado naendelea kuwaombea

wafanyakazi wenzangu kila ninapokuwa kwenye maombi.

Somo la 3: Mapepo yanaathiri hisia zako ili kukudanganya.

(Angalizo muhimu: Kabla ya kuendelea na Somo la 3, napenda

nikutahadharishe kabla kuwa somo ambalo Mungu amenifundisha

juu ya hisia ni gumu kuelewa kinadharia bila mtu kupitia mwenyewe

kile nitakachosema. Napenda kusisitiza pia kwamba sisemi kuwa

mawazo yote mabaya yanatoka kwa mapepo. Pia, sisemi kuwa

ni lazima wakati wote tujisikie vizuri na tujisikie kuinuliwa. Sisi

binadamu ni viumbe wa hisia sana na tunaathiriwa na hali ngumu

na matokeo yake tunapata hisia za aina mbalimbali.

Hata hivyo, kuna nyakati ambapo hisia zetu hasi zinakuja

kutoka kwa mapepo moja kwa moja. Ni lazima wakati wote

tutafute mwongozo wa Mungu na kumwomba atufundishe jinsi

ya kutofautisha kati ya hisia zinazotoka kwetu na ambazo ni

mashambulizi ya mapepo na tumwombe atufundishe jinsi ya

kupambana na mapepo yanayotuletea hisia mbaya).

Nimejifunza kuwa mapepo yana uwezo wa kuathiri hisia zetu kwa

kutumia huzuni, kukata tamaa, kujiona hatuna maana, kuhisi kama

vile Mungu ametudanganya au ametuacha (na kwa upande wangu,

nilihisi kabisa kuwa Mungu amenisaliti) kuhisi kama vile Mungu si

wa kuaminiwa au Neno lake si la kuaminiwa, kuhisi Mungu hasikii

maombi yetu, achilia mbali kujibu; kuhisi kuwa Mungu hatupendi;

kwamba tumeshapoteza wokovu wetu, au kama tumemkasirikia

sana Mungu, kuhisi kuwa Mungu hatatusamehe, nk. Lengo la

mapepo ni kukuibia wewe na mimi furaha ya wokovu wetu ambayo

imo ndani ya mioyo yetu. Nimejifunza kupambana na uongo na

kusimama kwenye kweli ya Injili (furaha na amani nilizopewa

na Yesu katika roho yangu) badala ya kukubaliana na nguvu ya

udanganyifu ya mapepo inayotaka mimi niamini hisia zangu badala

ya kuamini Kweli na Neno la Mungu ... na kufanya Neno la Mungu

liwe ndiyo lenye mamlaka ya mwisho kwenye kila jambo.

Nakumbuka wakati fulani wa majira ya joto ambapo nilirudi

kazini nikiwa nimekata tamaa kabisa na nikayaona mapepo

yamenizunguka yakirukaruka kwa furaha kwa sababu hiyo. Jambo

hilo lilinighadhibisha mno Kama kuna kitu ambacho sikuwa tayari

nacho ni kuyapa mapepo nafasi ya kushinda na kufurahia kwenye

maisha yangu. Kwa hiyo, nilichofanya ni kuyatazama, nikavuta

pumzi kwa nguvu, nikala chakula cha jioni, kisha nikakusanya

nguvu zangu zote nilizokuwa nimezipoteza na nikasema kwa sauti:

“Mungu, asante kwa kazi na asante kwa furaha na amani niliyonayo

kwenye moyo wangu.” Nilienda chumbani kwangu na kuanza

kusoma Maandiko kwa sauti. Baada ya hapo sikuyaona tena yakiwa

yanarukaruka kwa furaha.

Nakumbuka pia wakati mwingine mapepo yalikuwa

yananishambulia kwa hisia za kukata tamaa pamoja na huzuni

kubwa. Nilishindana nayo sana. Huwa hayatumii sana mbinu hiyo

kwangu. Haina nguvu sana kwa sababu huwa najitahidi kutofuata

KAMWE hisia zangu. Huwa sisomi Biblia kwa vile tu eti NAJISIKIA

kufanya hivyo au kuomba kwa vile najisikia kufanya hivyo.

Ninasoma Neno na kuomba kwa sababu nimeamuriwa kufanya

hivyo na kwa sababu ninataka kuonyesha uaminifu wangu

kwa Mungu. Ninapotambua kuwa mapepo yananishambulia kwa

hisia hasi, mara moja ninamshukuru Mungu kwa ajili ya furaha na

amani niliyonayo katika roho yangu, nayakemea, kisha naendelea

na kile ambacho nilikuwa nimepanga kufanya.

Lengo kuu la mapepo katika kushambulia hisia zangu ni kutaka

kunidhibiti kupitia hisia. Sasa kama sitazifuata hisia zangu, lakini

nikafuata Neno la Mungu, mashambulizi yao yanakuwa ni kazi bure.

Ninajua kuwa mapepo huathiri si tu hisia zetu kwa kutujaza hisia

hasi, bali pia kwa kutumia hisia chanya za bandia ambazo ni

rahisi kwa mtu kuzitafsiri kuwa ni uwepo wa Mungu. Nimejifunza

kuwa Mungu hatendi kazi kupitia hisia zetu. Mungu hutenda kazi

kupitia Neno lake na imani yetu tu. Mapepo mara zote hutenda

kazi kupitia hisia za mtu kiasi kwamba mtu huyo atasoma Biblia

na kuomba pale anapojisikia kufanya hivyo na si kwa vile Mungu

ameamuru afanye hivyo. Ni vibaya sana kwamba Wakristo wengi

hawatambui kuwa kujisikia vizuri wakati wa kuomba au kuabudu,

haimaanishi kuwa hisia hizo ni lazima ziwe zinatoka kwa Mungu.

Ni nadra kwa Mungu kufanya jambo ili tu kutufanya tujisikie vizuri

kihisia. Yeye ana malengo mengine tofauti kabisa kwa ajili yetu.

Anataka kutufundisha kujilisha mioyo yetu kwa kutumia Kweli

(Neno la Mungu). Kweli mara zote hukubaliana na roho inayotafuta

kumpendeza Roho Mtakatifu. Kwa roho zetu na Roho Mtakatifu

kutenda kazi kwa pamoja na kwa kukubaliana kabisa, hisia

zetu zitaanza kufuata mstari, na ndipo itakuwa rahisi kutambua

ni nanianayeendesha hisia zetu.

Wakati fulani nilihudhuria ibada kwenye kanisa fulani. Nilihisi

hali fulani ambayo mwanzoni nilikuwa nikiita ni “uwepo wa Roho

Mtakatifu.” Baada ya ibada nilimwendea binti mmoja. Aliniambia

kuwa alifurahia sana “uwepo wa Bwana.” Mara moja nilijiuliza swali,

“Ni kweli ni uwepo wa Bwana? Je, Mungu wangu ninayemtumikia

anawaita watoto wake ili wawe wakimya tu? Au Mungu wangu

anawaagiza watoto wake wawe macho na wawe waombaji muda

wote?”

Hivi karibuni Mungu amenifundisha nisikubali kabisa hisia za “uwepo

bandia wa Bwana” unaokuja kutoka kwa mapepo. Kwenye sehemu

ya jumuiya ambako watu wanatafuta kuwa kwenye uwepo wa

Mungu, muziki wa sauti kubwa, kupaza sauti kwa watu pamoja

na spika kunaweza kusiwe chochote bali ni uchocheaji wa hisia

zetu hadi kiwango cha juu kiasi kwamba kunaweza kudhaniwa

kuwa ndio “uwepo wa Mungu” wakati siyo. Na inapotokea hivyo,

shetani anaweza kuleta udanganyifu kwa kila namna unaoweza

kuonekana kama ni utendaji kazi wa Roho Mtakatifu kumbe Roho

Mtakatifu anaweza kuwa yuko uani anatapika (yaani anaweza

kuwa anajisikia kinyaa kwa hali kama hiyo). Uwepo wa kweli wa

Mungu huwa unatambulika kwa mtu mmojammoja peke yake –

kwenye utulivu – katika ushirika binafsi na Mungu. Yesu hakuwa na

haja ya kuchochea watu kihisia kwenye sehemu ya watu wengi ili

kusikia kile ambacho Baba yake alitaka afanye. Mara zote ilikuwa ni

kwenye utulivu, mahali ambako hakuna vurugu. Hapo ndipo aliona

“uwepo wa Mungu.”

Lakini imekuwa ni kinyume chake ambapo kundi la Wakristo

“husubiri kwa kimya uwepo wa Roho” uwatembelee.

“Watetemekaji” na "wachekaji" na "waliaji" wamekuja na

kupita; na watakuja na kupita ... na kama udhihirisho wa nguvu

unaotokea wakati huo, hauzai matunda yaliyo wazi kwa dhambi

kuwekwa wazi na kutubiwa – roho haziokolewi – hakuna huduma

inayoburudisha ya Neno la Mungu – hakuna uponyaji wa hakika

ambao umethibitishwa na wataalamu wa afya – watu wanaanguka

kwa kile kinachodhaniwa kuwa ni nguvu za Mungu, kitu ambacho

hakifanyi lolote zaidi tu ya kuvutia machoni mwa watazamaji.

Mapepo yanapewa uwanja wa kudhihirika kwa “wakristo” kwenye

ibada bila ya Wakristo hao kufuatiliwa kibinafsi. Wakristo ni lazima

wawe makini sana kukubali kwamba “miujiza hiyo inatoka kwa

Mungu.” Japokuwa Mungu amefanya na ataendelea kufanya yote

hayo niliyotaja hapo juu, shetani naye anaweza, na ataendelea

kuigiza mambo hayahaya.

Nimegundua kuwa mara mashambulizi ya adui yanapotambulika na

mtu akapambana nayo kwa bidii zote kwa kutumia upanga (Neno)

na ngao (Imani), adui huondoka mara moja. Ashukuriwe Mungu

atupaye kushinda kupitia Bwana wetu Yesu Kristo (1 Kor. 15:57) na

ambaye hutufanya kushinda (2 Kor. 2:14).

Kutambulishwa kwenye vitabu vya Rebecca Brown

Baada ya kutambua jinsi adui yangu alivyo na nguvu na ukatili,

niliamua kujifunza zaidi kuhusu vita vya kiroho kutoka kwenye

vitabu vya Kikristo mbali na kujifunza Biblia na kutoka kwenye

uzoefu wangu binafsi. Nilitambulishwa kwenye vitabu vya Rebecca

Brown na Mkristo mmoja kwenye kanisa nililoanza kuhudhuria mara

baada ya kuokoka. Nilitiwa moyo sana kuona kuwa kumbe mambo

mengi niliyojifunza katika vita vyangu vya kiroho yanathibitishwa

na Rebecca katika kitabu chake. Kupokea uthibitisho wa uzoefu

wangu limekuwa ni jambo muhimu sana kwangu kwa kuwa sikuwa

na mtu yeyote ambaye ningeweza kumshirikisha uzoefu wangu.

Zaidi ya hapo, ilikuwa ni muhimu pia kwangu kutambua kuwa

sikuwa peke yangu niliyeshambuliwa na adui. Wapo watoto wengi

wa Mungu wanaopitia mashindano makali kama yaleyale. Kujua hili

kumenisaidia kunyamazisha sauti ya adui aliyekuwa akininyanyasa

kutokana na ukweli kwamba “niko mpweke na peke yangu na sina

marafiki.” Kwa neema ya Mungu, hathubutu kufanya hivi tena,

maana ninajua kuwa siko mpweke (Yesu yuko nami daima) wala

siko peke yangu (watoto wengi wa Mungu nao pia wanashindana na

adui). Japokuwa sina marafiki wa Kikristo waliokomaa hapa Moscow

muda huu ninapoandika, najua kuwa hili limepangwa na Mungu

kama sehemu ya mafunzo yangu ili nijifunze kumtegemea Yeye

kunifundisha jinsi ya kufanya vita vya kiroho vyenye ushindi dhidi

ya nguvu za kipepo. Nisingependa watu wapate picha kwamba "ni

mimi naYesu tu"; kwamba siwahitaji Wakristo wengine kutoa

mchango kwenye maisha yangu, na kuniombea mimi pamoja na

mwito wa Mungu maishani mwangu - hapana. Isipokuwa kwamba

kwa sasa niko kwenye kipindi ambacho Mungu ananifundisha

mambo mengi moja kwa moja kutoka kwa Roho wake. Ni Mungu tu

ajuaye kile kitakachotokea kwenye maisha yangu yajayo.

 Udanganyifu wa shetani makanisani

Baada ya kusoma vitabu vya Rebecca nilifanya utafiti kwenye

mtandao wa Google na kuiona tovuti yake. Kwenye tovuti

hiyo nilikutana na unabii/maono mawili kuhusiana na uchaguzi

mbalimbali wa Marekani yaliyoandikwa na mume wa Rebecca,

Daniel. Nilishtuka sana baada ya kufahamu kuhusu mbinu za adui.

Nimeshahuhudia uthibitisho mwingi kote kwenye habari za dunia

na kanisani kwamba unabii wa Daniel ulikuwa kweli kwa 100% na

unatoka kwa Mungu. Macho yangu yamefunguka na kuona kazi ya

adui iliyo ya kificho sana dhidi ya kanisa ikiwa ni pamoja na:

-        Maombi yaliyojaa ubinafsi na kujitazama mwenyewe tu.

-        Mahubiri yanayolenga upendo wa Mungu kama njia ya kunufaika sisi

na kile ambacho Mungu anaweza kututendea na si kile tunachoweza

kutenda katika kumtumikia na kuenenda kwa utii mbele zake.

-        Unabii kuhusina na upendo wa Mungu usiokoma na si kuhusu haja

ya kuacha dhambi na kuwajali waliopotea.

-        Mara chache sana nimesikia makanisani kwamba Wakristo

watateseka kwa ajili ya Yesu (na kiukweli, kadiri wanavyojitoa

kwa bidii kwa Mungu ndivyo huenda watateseka zaidi isivyo haki);

kwamba wanatakiwa kutambua na kujifunza kuukana ubinafsi wao;

kwamba mateso ni jambo linalotokea kila siku kwa namna moja au

nyingine na kwamba wanatakiwa kubeba misalaba yao ya mateso

yasiyo ya haki yatokanayo na kuonewa na kumfuata Kristo bila

kujali kuna maumivu kiasi gani – bila kujali gharama inayotakiwa.

-        Kile ambacho nimeona kuwa kinasikika zaidi ni ujumbe wa

kificho wa kile ambacho Mungu atanitendea kama nikifuata kwa

usahihi “kanuni” fulani fulani na si kile ambacho ninatakiwa

kufanya kwa ajili yake ili kuenenda katika utakatifu na kuachana na

ubinafsi wangu ili kuwasaidia wengine kuja kwa Mungu na kukua

ndani ya Mungu.

 Gharama ya kuwa Mwanafunzi wa Yesu

Septemba iliyopita, nilijitolea kufundisha masomo ya Biblia ili kutoa

picha ya gharama ya kuwa mwanafunzi wa Yesu pamoja na vita

vya shetani dhidi ya Wakristo. Nilichagua mistari inayojibu maswali

yafuatayo:

•            Je, Yesu anaahidi utajiri kwa wanafunzi wake?

•            Je, Yesu anaahidi afya kamili ya kimwili kwa wanafunzi wake?

•             Je, ahadi ya kuteswa na kuteseka ilitimia kwenye maisha ya

Wakristo wa Agano Jipya?

•            Je, Mungu anavumilia dhambi kwenye maisha ya Mkristo? Kwa nini

Wakristo waliteswa?

•            Kwa nini Neno la Mungu linasema kuwa kila anayetaka kuishi

maisha ya uchaji Mungu atateswa?

•            Je, Mungu anamruhusu shetani kuwashambulia Wakristo moja kwa

moja?

Niligundua kuwa wakati nikisoma Maandiko haya baadhi ya

watu walikosa utulivu. Nilipofika kwenye kusoma Maandiko

yanayoongelea kuhusu shetani kumpepeta Petro kama ngano,

kijana mmoja alipayuka kwa hasira. Alipinga kabisa mimi kusoma

mstari huo. Alisema kuwa mstari haukuwa unahusiana kwa namna

yoyote na Petro kumkana Yesu, na hakuniruhusu kuendelea kusoma

Maandiko zaidi ili kufafanua mstari huo. Nilikuwa sijawahi kukutana

na upinzani mkali namna hiyo kwa Neno la Mungu kutoka kwenye

kundi la waamini, na sikutaja chochote kinachonihusu mimi binafsi.

Nilikuwa nasoma tu kutoka kwenye Neno la Mungu!

Nilipomwomba kijana yule aniache angalau niendelee kusoma

Maandiko, alisema kuwa hataruhusu mafundisho yoyote ya uongo

kwenye kundi letu dogo. Wanakikundi wengine nao walinikabili na

kunitaka niwaeleze sababu hasa ya mimi kuwasomea mistari ile.

Karibu wakimbie kabisa kutoka kwenye nyumba yangu ungedhani

mimi ni mchawi. Niliumia na kulia.

Baada ya siku chache, Mungu alisema nami.

Aliniambia:“Watalikataa jina lako kama uovu. Thawabu yako ni

kubwa mbinguni. Niamini Mimi tu, Neno langu tu. Nitakuja na

kumlipa kila mmoja kwa kazi yake. Waombee. Vifungo nilazima

viharibiwe kwanza. Vifungo ni:

•      Mwili

•      Kupenda mali

•      Kujipenda mwenyewe

•      Starehe

Utateseka, usijipende mwenyewe, jikane mwenyewe, jifunze

kujikana katika kila kitu kinachopingana na Mimi. Soma Neno langu

na kuomba kila wakati. Nitajitukuza kupitia wewe. Hii itakuja kupitia

maumivu na mateso utakayopitia. Jifunze kuridhika na ulicho

nacho. Nataka kuwa chanzo pekee cha furaha yako na ridhiko.

Asiwepo mwingine. Omba kwa ajili ya kuenea kwa Neno langu

na kuharibiwa kwa kazi za adui. Jifunze kuniamini Mimi. Jifunze

kufurahi kwenye mateso yako. Omba kwa ajili ya kuharibiwa kwa

uongo na udanganyifu unaoharibu akili za wanangu. Nawapenda

wote sawasawa. Jiachie kwenye mapenzi yangu. Utukufu ni wa

kwangu peke yangu. Omba kila wakati, omba. Uharibifu unakuja

kwenye dunia hii. Wale wanaonitumikia ndio watakaopona; wale

wasionitumikia hawatapona. Omba.”

Baadaye nilipata uthibitisho ufuatao kwenye Neno la Mungu.

2 Timotheo 3:1-5:

Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho

kutakuwako nyakati za hatari.

Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye

kupenda fedha, wenye kujisifu,

wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao,

wasio na shukrani, wasio safi, wasiowapenda wa kwao,

wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali,

wasiopenda mema,

wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko

kumpenda Mungu;

wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao

nao ujiepushe nao.

Nguvu ya Mungu inatolewa si tu kuokoa, bali pia kuponya na

kukomboa na kuua asili yetu ya ubinafsi, anguko na kukosa

utii ...sio tiketi ya kusamehewa tena na tena huku mtu anaendelea

kutenda dhambi ileile tena na tena na kuyapuuza kana kwamba

toba ndogo tu inatakiwa kufanya kila kitu kiwe sawa kati yetu na

Mungu, halafu mtu anarudi tena kuyafanya matendo hayo hayo ya

uasi hadi atakapoenda tena kutubu. Unakuwa ni mduara unaojirudia

tena na tena kama kwamba Ukristo si zaidi ya kusema: "Unajua

nini? Naweza kutenda dhambi na ilimradi ninatubu, naweza kufanya

dhambi ileile tena na tena na kila kitu kinakuwa sawa tu kati yangu

na Mungu! Napenda kweli aina hii ya Ukristo!”

Hapana! Haitakiwi kuwa hivyo!

Tangu niokoke, nimekumbana na mashambulizi kadhaa kutoka kwa

adui ambayo yanakuja kupitia kwa mtu tunayekaa naye chumba

kimoja, wafanyakazi wenzangu, na hata washirika wa kundi langu

dogo la wapendwa, japo ndiyo yanakuja kutoka kwenye tamaa

za mwili wangu. Adui anatumia kila kitu na kila mtu kunijaribu

na kujaribu kuniharibu. Nimejifunza kuwa Yesu kweli alimaanisha

pale aliposema: “Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane

mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate.” (Luka 9:23).

Wakati mapambano yangu yanapokuwa makali kabisa, wakati

mwingine nahiksi kama vile msalaba wangu ni mzito kupita kiasi.

Ni vigumu sana kushinda mashambulizi ya mara kwa mara ya

adui, lakini Mungu amekuwa kila wakati mwaminifu na hunipatia

mstari unaofaa wa kumnyamazisha adui na amenipa hekima ya

kujishusha mbele zake na kutofunua kinywa changu mbele za wale

wanaonizushia mambo ya uongo.

Hivi karibuni nimegundua kwamba hata kwenye mapambano

makali, pale ambapo kila kitu na kila mtu anakuwa kinyume

nami INAWEZEKANA kubakia na furaha na amani ambayo Yesu

anatuahidi kwenye roho zetu, hata kama sijisikii furaha na amani

kihisia. Mapepo yanaweza tu kunidhuru kimwili na kihisia, lakini

kama nikisimama kwenye Neno la Mungu, hawawezi kunidhuru

moyo wangu ambako ndiko anakokaa Mungu. Neno la Mungu,

maombi na imani NI SILAHA ZENYE NGUVU SANA dhidi ya adui.

Kuingilia himaya ya shetani

Novemba 2004, nilikutana na jambo ambalo lilinipa msukumo wa

kujifunza zaidi kuhusiana na ibilisi na imani za siri. Nilisoma makala

kwenye gazeti kuhusiana na tovuti fulani ya Kirusi ambayo ilikuwa

inahamasisha watu kujiua. makala hayo yalikuwa yanahusiana na

vijana waliokuwa na majonzi na mawazo ya kujiua ambao hatimaye

walijiua kutokana na ushawishi wa tovuti hiyo. Makala yalisema

kuwa tovuti hiyo ilikuwa na taarifa nyingi za namna ambavyo

mtu anaweza kujiua kwa mafanikio. Vijana kadhaa waliosaidia

kuitengeneza tovuti hiyo, baadaye walikutwa wakiwa wamekufa.

Wazazi wao walimshitaki kiongozi/mwanzilishi wa tovuti hiyo.

Baada ya kusoma makala niliamua kuitazama tovuti hiyo. Nilikuwa

sijui kabisa kwamba tovuti hiyo ilikuwa ina uvuvio wa shetani na

kuendeshwa na waabudu shetani. Tovuti hiyo ni ya uovu kamili

ikiwa na picha za watu waliokufa na mandhari yenye giza ambayo

yanamfanya mtu asiyekuwa na huzuni au mfadhaiko aupate. Mbali

na mwonekano wa ajabu wa nje, tovuti hiyo unatoa giza la kiroho

ambalo linawaathiri moja kwa moja watu wanaoitembelea.

Nilisoma maelezo kuwahusu watu kadhaa humo ndani.

Wote walikuwa na historia zinazofanana. Walikuwa ni watu

walionyanyaswa sana wangali watoto; walitoka kwenye ndoa

zilizovunjika; walikataliwa na wazazi wao wakiwa wadogo;

hawajawahi kupata upendo au matunzo ya wazazi. Niliamua

kwenda kwenye sehemu ya kutoa maoni ili angalau niweze kusema

nao kwamba kuna mmoja anayeweza kuponya maumivu yao

na kuwaweka huru mbali na huzuni na fadhaa zao. kwa kutojua

kwangu, nilidhani kuwa huenda naweza kuwafikia watu wale.

Mtu mmoja akawa amevutiwa na kile nilichosema na akataka

kufahamu zaidi kuhusiana na kuwekwa huru. Hata hivyo, nilipoanza

kumweleza kuhusu kweli za Biblia, kila mara nilipoandika jina la

Yesu Kristo lilifutika. Kwa siku nzima nilizuiwa kabisa kuchangia

chochote kwenye ukurasa huo.

Usiku wa kwanza baada ya kuchangia kwenye tovuti ile, nilipatwa

na jinamizi baya sana! Mungu aliniamsha katikati ya usiku na

akaniambia niombe. Nilijawa na hofu kubwa kutokana na uwepo wa

uovu chumbani kwangu.

Siku iliyofuata nilijisikia kichefuchefu. Nilienda kwenye tovuti

ile asubuhi. Msichana mmoja aliandika swali, akiuliza ni dawa

gani atumie na ni kwa kiasi gani ili aweze kujiua. Nilijaribu

kumtumia ujumbe ili kumwambia amwite Yesu. Ujumbe wangu

ulizuiwa kwenda. Msichana yule alipata ujumbe kutoka kwa mtu

mwingine ukimshauri atembelee sehemu nyingine kwenye tovuti

ile inayoeleza kwa undani namna mbalimbali za kujiua. Nilitambua

kuwa, kwa makusudi, nilikuwa nimezuiwa kabisa kuandika ujumbe

wowote kwenye tovuti ile.

Niliamua kuwaeleza kundi lile letu dogo la maombi ili tuombe dhidi

ya ile tovuti na kwa ajili ya watu na kwa ajili yangu (maana nilianza

kupata majinamizi). Hata hivyo, hadithi yangu iliamsha chuki na

hasira nyingi! Wanakikundi walinizuia kwa ukali kuzungumzia

tena kuhusiana na tovuti ile na wakaanza kuhoji kama na mimi

nilikuwa na mawazo ya kutaka kujiua, na kama kweli nilikuwa

nimekombolewa kutoka kwenye mfadhaiko. Sikuamini kile

nilichokuwa nakisikia kutoka kwao!

Kisha kwa ukali waliniambia niondoke kwenye kikundi kile cha

Biblia kama nilikuwa sipendi vile walivyokuwa wakiomba sana kwa

ajili yao kibinafsi na kwa ajili ya wanakikundi wenyewe. Nilikuwa

sijawahi kutamka chochote juu ya kuondoka kwenye kikundi. Ni

wazi kwamba niliumia sana, nikalia na nikajaribiwa kuinuka na

kuondoka zangu. Hata hivyo, Mungu aliweka ndani yangu moyo wa

kubakia, kwa hiyo nilibakia pale.

Nilifurahi kwamba nilibakia kwa sababu mama mmoja mtu mzima

aliomba kwa ajili yangu. Aliniambia kuwa niliingia kwenye himaya

ya shetani bila ya kuambiwa na Mungu. Alinishauri kuwa niombe

tu kwa ajili ya watu wale wa kwenye tovuti, lakini akashauri kwa

nguvu sana kwamba niache kutembelea tovuti ile. Nilielewa kuwa

alikuwa sahihi. Nilijua kuwa siwezi kushindana na uovu niliokutana

nao. Haikuwa ni mashambulizi tu ya kawaida. Hapana. Ilikuwa

ni zaidi ya hapo – uovu mkubwa ambao usingekaa kimya kwa

sababu nimeingilia himaya yake. Nilizingatia ushauri wake. Hata

hivyo, majinamizi, hofu kubwa na uwepo wa uovu usiku viliendelea

kuniandama kwa muda.

Miezi miwili baadaye nilikuja kufahamu kuwa baadhi ya watu

wanaoendesha tovuti ile ni waabudu shetani. Kama ningejua hilo

kabla, nisingejaribu hata kuifungua tovuti ile. Namshukuru Mungu

kwa kuniweka salama wakati wa kukosa kwangu umakini. Mungu

aliniambia niendelee kuwaombea wale walio na mfadhaiko na kwa

ajili ya kuharibiwa kwa tovuti ile.

Baada ya tukio lile, niliamua kuijifunza mengi kadiri iwezekanavyo

kuhusiana na vita vya kiroho na adui na wale wanaojihusisha na

imani za siri. Najua kuwa kuingilia himaya ya adui bila mwongozo

wa moja kwa moja wa Mungu kunaweza kuwa ni jambo la hatari

sana. Katika kutafuta kwangu kufahamu juu ya ulimwengu wa

kipepo, nilinunua maandiko ya Howard Pittman, Jessie-Penny

Lewis na Rebecca Brown. Ninapendekeza kila Mkristo asome

kitabu kilichoandikwa na Jessie-Penn Lewis. Ni moja ya vitabu

vilivyoandikwa kwa uzuri na kwa undani kuhusiana na mambo

ya ulimwengu wa roho, kama ambavyo wengine wengi nao

wanakubaliana na hili. Nadhani Wakristo wote wanaweza kupokea

mafunuo mengi kupitia kitabu hiki, nacho kinaweza kupatikana kwa

kubofya: Hapa

Ufupisho wa masomo niliyojifunza kutoka kwa Mungu

Kwa kifupi, Mungu alinifundisha mambo yafuatayo:

1.   Kila Mkristo amepangiwa mapepo na shetani yanayomfuatilia ili

yamharibu. Hakuna asiyekuwa nayo. Mungu kwa upande wake

ametupangia malaika mmoja au zaidi wa kutusaidia. Kama

tungeruhusiwa kuona ulimwengu wa roho unaotuzunguka, tutaona

malaika na mapepo wametuzunguka.



2.   Mapepo hutufuata kila wakati. Wanafahamu udhaifu wetu, hivyo

wanapanga kutushambulia katika muda ulio mwafaka kwao. Ni

muhimu kwangu kufahamu udhaifu wangu na kumwomba Bwana

augeuze kuwa nguvu kwangu. Kujikana mwenyewe na kuachana

na kila kitu ninachokipenda sana ambacho hakimtukuzi Mungu

ni jambo la lazima. Ni njia pekee ya kupunguza uwezekano wa

kushambuliwa na adui.



3.   Lengo la mapepo ni kunifanya nimuasi Mungu, kunifanya niwe mtu

wa kumnung’unikia, kumlalamikia, na kumkasirikia Bwana wangu

Yesu, na kuwadharau watu wa Mungu wasio na sifa mbalimbali.

Nilipogundua kuwa mateso na matatizo yangu yanatoka kwa adui

na si kwa Mungu, nilijifunza kuelekeza hasira zangu zote kwa

mapepo.



4.   Mbinu ninayotumia kumaliza hasira zangu kwa mapepo pale

yanaponishambulia ni kwa kujitahidi kufanya kile ambacho Mungu

ananiagiza kufanya na kutompa kabisa adui nafasi. Ninajua kile

ambacho adui anataka kwangu na mimi siko tayari kumpatia kwa

hiyari yangu mwenyewe. Ni wazi kuwa haya ni mapambano makali

na magumu. Namjua yule ninayekabiliana naye; ni kiumbe mwenye

nguvu zaidi baada ya Mungu. Ni adui mwovu kabisa ambaye

mwanadamu anaweza kuwa naye hapa duniani. Sitarajii haki

yoyote kutoka kwa adui. Sitarajii kuwa ataniruhusu tu nisababishe

madhara kwenye ufalme wake kisha niendelee kuishi kwa furaha

tu hapa kwenye ufalme wake duniani. Nimeshahesabu gharama

zangu. Kila kitu maishani mwangu kiko hatarini. Najua kuwa adui

daima anadai, ama moja kwa moja au si moja kwa moja, ili Baba

amruhusu, yeye ibilisi anijaribu. Na pale ruhusa inapotolewa, najua

kuwa ibilisi atanivuta kuliko uwezo wangu. Lakini pia najua kuwa

Mungu ameahidi kuwa atanisaidia kushinda na kustahimili. Yesu

hakuwahi kuahidi kuwa ataniepusha na mateso, lakini aliahidi kuwa

atanifundisha kushinda na kustahimili. Niko tayari kubeba msalaba

wangu kila siku hadi mwisho, kushinda na kustahimili. Pia niko

tayari kupokea thawabu nzuri kwenye ufalme wa Mungu. Katika vita

vyangu siko tayari kurudi nyuma – sina mahali popote pa kurudia

nyumba – nina kusonga mbele tu!



5.   Hakuna kitu kinachotetemesha ufalme wa shetani na jeshi lake la

mapepo kama pale watoto wa Mungu wanapoendelea kushikilia utii

wao kwa Bwana Yesu kupitia kumshukuru kila wanapoteswa na

kufedheheshwa na adui. Mungu amewapa mitume wake , maandiko

mengi "kuhesabu kuwa furaha" tunapoteswa isivyo haki na shetani

na kustahimili, maanathawabu yetu itakuwa kubwa mbinguni.

(Ibilisi muda wote anataka tuhisi kuwa Mungu ni katili kwa sababu

hatupatii thawabu zile tunazotaka kwenye maisha haya; na ni

lazima tuwe waangalifu ili tusiingiwe na hisia za kujionea huruma

kama kila kitu kinaonekana kiko kinyume nasi; vinginevyo ibilisi

anaweza kutumia hali hiyo kufanya shauku yetu ya kumtumikia

Mungu ishuke chini).



6.   Kumbuka ... maisha haya ni mafupi mno kulinganisha na milele.

Mateso yoyote ambayo Mungu anaruhusu tuyapitie kwa miaka

michache hii tuliyo nayo hapa duniani, hata kama ni makali kiasi

gani, hayawezi kulinganishwa na uzito wa milele wa utukufu

yatakayotuletea. Hilo ni Neno la Mungu! (Tazama: 2 Kor. 4:17-18).

Kwa wale wanaojiona wamesalitiwa na Mungu

Kama kuna kipindi ulikuwa na moto na Mungu, ukiomba kwa bidii

na kusoma Biblia kwa bidii, lakini kidogo kidogo umeingiwa na

uchungu dhidi ya Mungu kwa sababu ya matatizo au mateso na

dhiki, mambo yafuatayo ni kwa ajili yako kibinafsi.

Kwa kuwa na mimi nimepita mahali uliko hivi sasa, na ninafahamu

uchungu wa kihisia na mfadhaiko unaokutesa, ningependa

kukupatia hatua kadhaa ambazo zilinisaidia mimi kupata uhuru

kutoka kwenye nguvu za shetani.

Njia yangu kuelekea kwenye kukombolewa:

1. Mungu alinisaidia kutambua kuwa Yesu hanichukii wala hanilaani.

Nilienda kutazama sinema ya “Mateso ya Kristo”. Kwa kutazama

mateso ya Kristo nilitambua kuwa Kristo hakunichukia hata kidogo.

Mapepo yalinishawishi kwamba Mungu alinichukia na kunilaani na

kwamba Yesu hakupata mateso makubwa ya kihisia. Uongo wao

uliota mizizi kwenye akili yangu. Niliteswa na uongo huu kwa miaka

miwili. Kupitia sinema ile, Mungu alivunja nguvu ya giza lile kwenye

akili yangu. Nilitambua kuwa Yesu, si tu kwamba hakunichukia, bali

pia aliteseka sana kwa ajili yangu. Hii ilikuwa ni hatua yangu ya

kwanza na ya muhimu sana kuelekea kwenye uhuru wangu.

2. Kwa kusoma shuhuda za waliookoka, nilielewa kuwa kumbe

sikuwa peke yangu kwenye mateso na dhiki. Kabla ya kuja kwa

Kristo, watu wengi walipitia mateso makali zaidi kuliko ya kwangu.

Mwanzoni mwa mchakato wa ukombozi wangu, mapepo yalishikilia

kwa nguvu sana akili yangu kiasi kwamba sikuelewa Biblia na

sikuweza kustahimili kusikiliza au kusoma Neno la Mungu. Hata

hivyo, nilikuwa na shauku ya kutaka kujua kama kulikuwa na

Wakristo wengine waliokuwa na mapito kama yangu. Wakati

nikitafiti kwenye mtandao wa Google, Mungu aliniongoza kwenye

tovuti ya Shuhuda za Thamani (www.precious-testimonies.com).

Wakati ninasoma shuhuda, Mungu alivunja uongo mwingine

uliokuwa umejikita kwenye akili yangu: nilitambua kuwa sikuwa

kamwe peke yangu kwenye mateso, kama ambavyo nilikuwa

nikiamini hapo kabla. Wapo wengi walioteswa zaidi yangu na

shetani. Kwenye shuhuda hizo, niliweza pia kuona namna shetani

alivyoharibu maisha ya wengine na jinsi Yesu Kristo alivyowaweka

huru na kuwapa maisha mapya.

Kweli kabisa “wao (Wakristo) walimshinda yeye (shetani) kwa

damu ya Mwana-Kondoo, na KWA NENO LA USHUHUDA WAO;

ambao hawakupenda maisha yao hata kufa. (Ufunuo 12:11).

Baada ya kutubu, niliamua kuyatoa maisha yangu yote kwa Kristo.

Nilitia saini agano langu la kwanza na Mungu ambapo niliachana na

ndoto zangu zote za duniani; shauku zangu na matumaini yangu.

Nilimpa Mungu haki zangu zote ili aamue iwapo niwe na kazi au

la; kama nitaolewa au la. Katika agano langu nilijitoa kumtumikia

Mungu bila kujali niko mwenyewe au nimeolewa; niwe na kazi au

sina.

Wakati nikisoma Maandiko baada ya kuokoka kwangu, nimegundua

kuwa sababu kuu ya mimi kuharibu imani yangu ni kuwa sikuwa

nimefundishwa kwa usahihi mafundisho ya Yesu Kristo. Katika

karne ya kwanza, Wakristo waliteswa na kufa kwa ajili ya Kristo na

HAWAKUMKANA Kristo. Mimi sikuwa nimepokea shauku za tamaa

zangu za kimwili ndiyo maana nikamkana Kristo!!! Unadhani hilo

liliwafanya shetani na mapepo wafurahi?

Katika karne ya kwanza Wakristo walifundishwa mafundisho

ya Kristo kuhusu kuvumilia mateso kwa ajili ya Kristo. Nilikuwa

sikufundishwa au kusikia juu ya kuhesabu gharama ya kumfuata

Kristo. Sikuwa nimesikia juu ya kustahimili mateso kwa ajili ya

Kristo au kwamba inanibidi nijikane mwenyewe, nibebe msalaba

wangu na kumfuata Kristo. Sikuwa nimesikia au kufundishwa

kwamba inabidi nikane ubinafsi wangu ili kumfuata Yesu (achilia

mbali kujifunza namna ya kubaini ubinafsi hasa ni nini!)

Badala yake, katika vitabu vya Kikristo nilijifunza mafundisho ya

mashetani kuhusiana na Mungu kutaka kunipatia kila kitu ambacho

moyo wangu unakitamani. Kwa namna fulani labda sikuona sura

kwenye vitabu hivyo ambayo inanionya kuwa Mungu hatanipatia

kila shauku ya moyo wangu kama shauku hizo ni za ubinafsi na

si sehemu ya mpango wa Mungu kwa maisha yangu. Ilikuwa ni

makosa yangu mwenyewe kuamini mafundisho ya mashetani.

Sikufanya kile ambacho Mungu ameniamuru kwenye Neno lake.

Sikuijaribu kila roho kwa Neno la Mungu na sikuwa makini na

manabii wa uongo na walimu wa uongo. Matokeo yake, niliamini

mafundisho mengi ya mashetani.

Ilikuwa ni makosa yangu kuamini kila kitu nilichosoma kwenye

vitabu vya Kikristo. Na pale Yesu alipoacha kutimiza shauku za

moyo wangu za kidunia, na pale matizo yalipokuja maishani

mwangu kama Yesu alivyoahidi katika Yohana 16:13, sikujua

namna ya kustahimili. Kwa hiyo mwishowe nilianguka.

Hatima ya mafundisho ya mashetani ni kuwadanganya wateule na

kusababisha imani yao kuharibika.

Yafuatayo ni mafundisho ya mashetani ambayo niliyaamini.

Mafundisho haya ya mashetani yako kwenye makanisa mengi,

vitabu, kanda na CD na kwenye intaneti:

1.   Kwamba Mungu anataka kukufanikisha kwa mali za kidunia na

kwamba ‘kuridhika na ulichonacho’ (Tazama: 1 Tim 6:8 na Ebr.

13:5) maana yake ni kuridhika na si chini ya dola milioni moja.”

2.   Kwamba Mungu anataka kukupa kila haja ya moyo wako, na

mapenzi yake kamili ni kujibu kila ombi utakaloomba – huku akijibu

kama wewe unavyotarajia ajibu.” (Kwa maneno mengine, hakuna

haja ya kutilia maanani ubinafsi).

3.   Kwamba shetani aliharibiwa kabisa msalabani, na kwamba shetani

hana nguvu juu ya maisha ya Wakristo. Hivyo, usipoteze muda

wako, hata wa dakika moja, kumfikiria. Vinginevyo, utakuwa

unampa utukufu ambao unamstahili Yesu.”

4.   Shetani amefungwa na hawezi kuwagusa au kuwadhuru Wakristo

– kwamba anachoweza yeye ni kudanganya tu. Wakati wa Ayubu

ulishapita kwa sababu Yesu alishamshinda shetani msalabani.

Hivyo, shetani hawezi tena kuwashitaki Wakristo mbele za Mungu.

Kwamba shetani hawezi kuchukua chochote tena kutoka kwa

Wakristo.

5.   Hauna haja ya kuteseka kwa ajili ya Kristo. Mateso si sehemu ya

Wakristo tena.

6.   Kila wakati Mungu anataka uwe mzima kimwili bila kutilia maanani

mambo mengine. Vipi kama Mungu anataka kumpeleka mtu

huyo mgonjwa nyumbani mbinguni? Vipi kama Mungu anataka

kumfundisha jambo ambalo kwa njia nyingine hawezi kujifunza;

kwa mfano kujifunza kumtukuza Mungu katika madhaifu yake?

Vipi kuhusu watu wanaoshiriki meza ya Bwana bila kujihukumu na

kujikagua wenyewe sawasawa? Maandiko yanasema kuwa watu

wanaweza kuugua na kufa wangali na umri mdogo kutokana na

kutojihukumu wenyewe sawasawa. (Tazama: 1 Wakorintho 11:29-

31). Inaonekana kwangu kwamba hekima inatutaka tuangalie

uponyaji wa kimwili kama tunavyoangalia dhambi. Tunajua kuwa

Mungu anataka dhambi yote iondolewe kwenye dunia, lakini hilo

halitatokea hadi baadaye huko mbeleni. Japokuwa tuko salama

kuamini kwamba uponyaji wa kila aina hakika umo ndani ya

upatanisho kwa ajili ya watu wa Mungu, ni lazima tuwe na hekima

ya kutomwacha shetani aharibu imani yetu pale tunapomtafuta

Mungu kwa ajili ya uponyaji ... hasa pale uponyaji huo unapogoma

kutokea licha ya kuomba kwetu kwa bidii.

7.   Kamwe usiseme, "Hata hivyo, si mapenzi yangu bali mapenzi ya

Mungu yafanyike maishani mwangu," kama hukupata kutoka kwa

Mungu kitu ambacho ulikiomba kwa Mungu. "Haujui mapenzi ya

Mungu kwa maisha yako, hivyo unatakiwa kuendelea kuomba zaidi

na zaidi ili Mungu akutendee kile unachokitaka.”

Yapo na mengine mengi zaidi – mafundisho ya kificho ya

mashetani yanayoendelea kufundishwa. KAMWE usiamini kila kitu

unachofundishwa kanisani au unachosoma kwenye vitabu vya

Kikristo kabla ya kukijaribu kama kinaendana na ushauri wa

Neno la Mungu katika Agano Jipya lote (pamoja na kanuni,

miongozo na amri za Agano la Kale ambazo hazipingani

na kweli iliyofunuliwa katika Agano Jipya, bali zinaiunga

mkono). Unafanyaje hivyo? Ibilisi anapenda kuchukua neno moja

au mawili kutoka kwenye Maandiko ambayo yanazua maswali

katika utekelezaji wake na kuyafanya yaseme kitu ambacho

Mungu hata hakukikusudia. Kila inapowezekana, acha Maandiko

yatafsiri Maandiko mengine. Acha hali ya kujirudia kwa mawazo

yaliyo kwenye Maandiko kujithibitishe kwenyewe ili kuumba imani

thabiti. Kutafsiri neno moja au mawili (au labda matatu au manne)

katika tafsiri zetu za Biblia za kileo kusichukuliwe kuwa ni lazima

kwamba kunaeleza kikamilifu maana iliyokusudiwa iliyokuwa

kwenye lugha za asili za Kiebrania na Kigiriki. Maneno, na namna

yanavyowasilishwa, yanaweza kubadilika kutoka utamaduni mmoja

hadi mwingine kadiri muda unavyopita. Roho Mtakatifu atathibitisha

kile kilicho cha muhimu kuamini na kipi sicho cha muhimu kutoka

kwenye Maandiko ili kumpendeza Mungu Baba kama tutanyenyekea

kiasi cha kutosha kukiri kuwa tunaweza kuwa tumekosea kutokana

na kile tunachoamini juu ya maeneo kadha wa kadha ya Biblia

ambayo hayaeleweki kirahisi.

Wakati huohuo, katika jitihada zetu za kuelewa na kutumia

sawasawa Neno la Mungu, tusisahau kamwe ukweli kwamba, ndicho

chanzo pekee cha kuaminika ambacho Mungu amewapa wanadamu

ili waweze kujua mapenzi ya Mungu. Neno la Mungu ndilo mapenzi
Mapenzi ya Mungu yamewekwa wazi kwenye Neno lake.

Hatuna cha kujitetea kwamba hatuwezi kujua mapenzi ya Mungu

yaliyowekwa wazi kwetu, (au miongozo ya namna ya kutafuta

mapenzi ya Mungu kwa ajili ya maisha yetu kibinafsi), kama hatujui

Neno la Mungu.

Huenda chapisho bora kabisa ambalo linaweza kumnufaisha sana

mtu katika kujifunza jinsi ya kujua kwa njia salama na ya hekima

kitu cha kuamini kuhusiana na Neno la Mungu linaweza kupatikana

kwa kubofya: Hapa.

Kumbuka, katika jamii tajiri, mafundisho ya mashetani ni nadra

sana kuwaambia watu kuwa ni lazima kuteseka kwa ajili ya

Kristo, ni lazima kumpinga shetani na ni lazima kujikana

mwenyewe, ubebe msalaba wako na kumfuata Kristo. Pale

ambapo kuna utajiri mwingi wa kimwili, mafundisho mengi ya

mashetani yana mvuto mkubwa kwa kimwili – karibu mara

zote huwa ni kwa ajili ya kile ambacho Mungu anaweza

kututendea na si kile ambacho tunatakiwa kutenda ili

kumpendeza Yeye.

Mafundisho ya mashetani karibu kila wakati huwa ni kwa ajili

ya kulisha tamaa zetu za kimwili, zenye ubinafsi; yanalenga

kupotosha maana na matumizi halisi ya Neno la Mungu; yanalenga

kushushia hadhi usahihi na uhalisi wa Neno la Mungu; yanalenga

kumpokonya Mungu utukufu anaostahili; yanalenga kuwadanganya

na kuwajaribu watu ili wamchukie Mungu wakati kumbe ni shetani

ndiye wanayetakiwa kumchukia.

Shetani anataka watu waamini kuwa jehanamu si halisi ili kusiwepo

na hofu yoyote ya Mungu na nia kuacha dhambi; kwamba mapepo

hawapo au kwamba hayana nguvu kabisa juu ya watu waliookoka

kwelikweli, maana kwa njia hiyo, Wakristo hawatamtafuta Mungu

kwa ajili ya kupewa uwezo wa kufanya kile wanachotakiwa kufanya

katika kusaidia kupambana na kazi za kipepo duniani na kwenye

maisha ya wapendwa wao. Orodha ya udanganyifu wa shetani

inaendelea na kuendelea ...

Shetani amejaribu, na hataacha kamwe kuendelea kujaribu,

kuwafanya watu wa Mungu wasitambue kuwa Neno la Mungu

lililoandikwa ndilo pekee lenye mamlaka ambalo Mungu analiafiki na

kulitia nguvu.

Hii ndiyo amri ya Mungu: Kwamba uyajaribu mafundisho yote

unayoyasikia kanisani au unayoyasoma vitabuni au kwenye

intaneti na kuwa makini na manabii wa uongo na walimu wa

uongo. Kama hujasoma sawasawa Agano Jipya bado, basi waendee

waelewa kadhaa tofauti wa Biblia wa kiprotestanti kabla ya

kuumba imani yako thabiti juu ya jambo lolote. Duka lolote la

vitabu vya Kikristo linaloheshimika linaweza kukutajia waelewa

hao. Kama hakuna duka karibu, bofya tovuti hii na kuwauliza.

Wanaaminika na wanaweza kukuelekeza kwenye mwelekeo

sahihi:www.gospelcom.net

1 John 4:1 Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho,

kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo

wengi wametokea duniani.

Philippians 3:2 Jihadharini na mbwa, jihadharini na watendao

mabaya, jihadharini na wajikatao.

Kumbuka: mafundisho ya mashetani yana uwezo mkubwa sana

ya kumharibu Mkristo kama ukiyaamini na kuyafuata. Mafundisho

ya mashetani yatakufanya usiwe na nguvu kwenye ufalme wa

Yesu na badala yake ukawa ni mtu wa kufuata tu ubinafsi wako au

yatafanya imani yako ife kabisa.

Shetani amejitoa kwa nguvu zote kufanya vita dhidi ya wafuasi wa

Kristo. Ni wale TU wanaofuata mafundisho sahihi ya Kristo ndio

wataweza kupona mashambulizi makali ya adui na kupokea “taji ya

uzima” kutoka kwa Mungu.

Ni lazima umwombe Mungu akufundishe jinsi ya kupambanua kati

ya uongo na kweli. Kumbuka kuwa kamwe hutaweza kushinda

uongo wa shetani kwa nguvu zako pekee. Ni kwa nguvu za Yesu TU

ndipo utaweza kuutambua uongo wa adui.

Nakutia moyo usome Biblia kwa bidii, kila siku. Mungu ndiye

Mwalimu BORA kabisa. Hakuna kitabu au mahubiri yoyote

yanayoweza kuchukua nafasi yote ya ushauri na mafundisho kutoka

kwa Mungu mwenyewe moja kwa moja. Shauku ya Mungu kwa

ajili ya watoto wake ni waijue kweli na kuweza kupambanua kati ya

jema na baya kama inavyosemwa kwenye Waebrania 5:14.

Mimi si pekee niliyeangukia kwenye uongo wa shetani; wako wengi

wanaopita kwenye matatizo kama niliyopitia mimi. Ni kwa sababu

tu ya rehema na neema kuu za Mungu ndiyo maana alinivuta nirudi

kwake na akanikomboa kutoka kwenye nguvu za shetani.

Ninamwomba Mungu atumie ushuhuda huu wangu kwa ajili ya

kueneza Ufalme wa Yesu na kuharibu ufalme wa shetani.

Endapo unanyanyaswa na nguvu za giza, au uko tayari kuachana na

Ukristo kwa vile unahisi kuwa Mungu amekusaliti, kama ambavyo

nami nilidanganywa na kuamini hivyo, unaweza kuniandikia

baruapepe. Nitafurahi kumtumikia Bwana wangu Yesu katika kujibu

maswali yako.

No comments:

Popular Posts